Shehena ya vipodozi vyenye viambata vya sumu vikiwa vinataka kusafirishwa kwenda Dar es salaam
Posted by tfdaakezone
Vipodozi vyenye viambata vya sumu vikiwa katika lori tayari kusafirishwa kwenda Dar es salaam. Vipodozi hivyo vilikamatwa na wakaguzi kufuatia msako mkali unaoendelea wa kukamata bidhaa zote za chakula,Dawa ,Vipodozi na Vifaa tiba ambazo hazijakidhi matakwa ya Sheria ya Chakula ,Dawa na Vipodozi namba 1 ya Mwaka 2003.
SHEHENA YA VIPODOZI VILIVYOPIGWA MARUFUKU KUTOKA NJE YA NCHI VIMEKAMATWA JIJINI MWANZA
Vipodozi vyote vilikamatwa na wakaguzi na zoezi la uteketezaji linaandaliwa kufanyika katika Dampo ya Buhongwa tarehe 24 Aprili 2013
OFISI YA MAMLAKA YA CHAKULA NA DAWA-MWANZA
Posted by tfdaakezone
Ofisi ya Kanda ya Ziwa ya Mamlaka ya Chakula na Dawa,TFDA iliyoko katika mtaa wa Nkurumah karibu na Benki ya Azania ,
Manispaa ya Nyamagana, Mkoa wa
Mwanza
MFANYABIASHARA ANAYEUSISHWA NA UTENGENEZAJI WA LEBO ZA DAWA NA KUTUMIKA KATIKA MAKOPO YA DAWA
Pichani ni Mfanyabiashara mmoja aliye chini ya ulinzi (pingu mkononi) kwa vile ‘Stationery’ yake ambayo aliuziwa na mfanyabiashara mwingine ilihusishwa na vitendo vya kutengeneza lebo za dawa na kutumika katika makopo ya dawa. Mtuhumiwa huyu alitoa taarifa zilizoweza kusaidia wakaguzi kupata alikohamia muhusika.
TFDA IKITOA ELIMU KWA UMMA KUHUSIANA NA SHUGHULI INAZOZIFANYA
Ofisi ya kanda ya Ziwa ikiwa katika moja ya maonyesho ikitoa elimu kwa uma kuhusiana na shughuli inazozifanya katika uthibiti wa usalama na ubora wa bidhaa inazozidhibiti zinazokuwepo katika soko la
Tanzania.
TAARIFA KWA UMMA KUHUSIANA NA OPERESHENI YA DAWA DUNI/BANDIA
Ofisi ya Kanda ya Ziwa ya Mamlaka ya chakula na Dawa imekua ikipata ushirikiano mzuri sana na jeshi la polisi katika kutekeleza majukumu yake,
Pichani ni Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya chakula na Dawa na pembeni yake ni Aliyekuwa kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza Hayati Liberatus Baro wakiwa katika shughuli ya kutoa taarifa kwa umma kuhusiana na operesheni ya dawa duni/Bandia iliyofanika katika Mkoa wa Mwanza mwezi Juni mwaka 2012.kufuatia zoezi hilo kesi 7 zilifunguliwa na watuhumiwa 13 walifikishwa mahakamani.
Pichani ni Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya chakula na Dawa na pembeni yake ni Aliyekuwa kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza Hayati Liberatus Baro wakiwa katika shughuli ya kutoa taarifa kwa umma kuhusiana na operesheni ya dawa duni/Bandia iliyofanika katika Mkoa wa Mwanza mwezi Juni mwaka 2012.kufuatia zoezi hilo kesi 7 zilifunguliwa na watuhumiwa 13 walifikishwa mahakamani.
MKURUGENZI MKUU WA TFDA AKITOA SEMINA KWA WAANDISHI WA HABARI
Ofisi ya Kanda ya Ziwa katika kutekeleza mpango kazi wake wa mwaka
2011/2012 iliandaa semina ya waandishi wa habari kutoka katika vyombo vya habari mbalimbali katika Mikoa ya Kanda ya Ziwa, ili kuweza kuwaongezea wana habari uelewa mpana kabisa katika kufahamu shughuli za Mamlaka
Pichani ni Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya chakula na Dawa ,TFDA aliyesimama na pembeni yake ni Mkururgenzi wa Dawa na Vipidozi, DMC akiwa anatoa maelezo ya utangulizi katika kufungua semina hiyo iliyofanyika katika ukumbi wa Nyakahoja,Manispaa ya Nyamagana Mwezi Julai Mwaka 2012
Pichani ni Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya chakula na Dawa ,TFDA aliyesimama na pembeni yake ni Mkururgenzi wa Dawa na Vipidozi, DMC akiwa anatoa maelezo ya utangulizi katika kufungua semina hiyo iliyofanyika katika ukumbi wa Nyakahoja,Manispaa ya Nyamagana Mwezi Julai Mwaka 2012
SEMINA KWA WAANDISHI WA HABARI
Pichani ni baadhi ya waandishi wa habari wakina wameshafika katika ukumbi wa Nyakahoja ulioko Mwanza Mjini tayari kwa semina hiyo.
UTEKETEZAJI WA BIDHAA
Ofisi ya Kanda ya Ziwa imekua ikiteketeza bidhaa za chakula, dawa, vipodozi na vifaa tiba zisizofaa inazozikamata katika soko, pichani ni mazoezi tofauti ya uteketezaji wa bidhaa za chakula na dawa maliyofanyika katika dampo la Jiji lililoko Buhongwa
TFDA KANDA YA ZIWA IKISHIRIKIANA NA WAJUMBE WENGINE KAMA TRA,UHAMIAJI NA POLISI
Ofisi ya Kanda ya Ziwa ikishirikiana na wajumbe wengine kutoka katika ofisi mbalimbali kama TRA, Uhamiaji, Polisi n.k watakaotumia ofisi mpya zinazojengwa katika kituo cha mpakani Mtukula kama ‘One stop boader post
(OSBP) wakiwa katika ukaguzi wa maendeleo ya ujenzi wa ofisi hizo ambapo mkandarasi aliahidi kuwa ifikapo mwezi April mwaka 2013 atakua amemaliza kazi.
VIPODOZI VYENYE VIAMBATA VYA SUMU
Bidhaa za vipodozi vyenye viambata vya sumu vikiwa vimekamatwa kutoka katika ghala la mfanyabishara vikiwa vimetoka kushusha kwa roli kutokea nchi jirani ya Kenya.Vipodozi hivi vilikamatwa na kesi ilifunguliwa
UKIUKWAJI WA UENDESHAJI WA BIASHARA YA DAWA
Ukiukwaji wa uendeshaji wa biashara ya dawa kiasi ambacho huduma za matibabu hutolewa katika maduka ya dawa ulipelekea mpango wa maduka ya dawa muhimu ambapo zaidi ya kwamba maduka haya kisheria yataweza kuuza baadhi ya dawa za cheti lakini pia watoa dawa watasoma na kuelewa umuhimu wa kufuata taratibu katika kuendesha biashara ya duka la dawa ambapo vitendo kama hivi katika picha vitatokomea kabisa.
Pichani ni duka moja Mkoani Kagera wilayani Karagwe likiwa na vifaa tiba vitendanishi na pia sindano iliyotoka kutumika kwa mgonjwa pembeni yake ilikutwa chupa ya penadur ikiwa imetoka kutumika.Duka husika lilifungwa.
Pichani ni duka moja Mkoani Kagera wilayani Karagwe likiwa na vifaa tiba vitendanishi na pia sindano iliyotoka kutumika kwa mgonjwa pembeni yake ilikutwa chupa ya penadur ikiwa imetoka kutumika.Duka husika lilifungwa.
KIWANDA KIKIPAKA RANGI KUTA,UZALISHAJI UKIENDELEA
Kiwanda kimoja cha Biscuits Mwanza Mjini kilikutwa kinapaka rangi baadhi ya kuta zake eneo la uzalishaji wakati shughuli za uzalishaji wa biskuti zikiwa zinaendelea.Kiwanda husika kilifungwa na kutakiwa kumaliza shughuli za kupaka rangi kabla uzalishaji haujaendelea.Pembeni ni makreti ya biskuits ambazo zilizuiliwa.
TAFRIJA YA KUAGWA KWA ALIYEKUWA MENEJA WA KANDA-TFDA
Tafrija ndogo ya chakula cha jioni iliyofanyika katika ukumbi wa hoteli ya JB Delmonte ya kumuaga aliyekua Meneja
wa Ofisi ya Kanda ndugu Seth Kisenge na kumkaribisha Kaimu Meneja Mpya Ndugu Moses
Mbambe
Subscribe to:
Posts (Atom)
Powered by Blogger.