LakeZone Office

Nkurumah Street PO BOX 543 MWANZA Tel: +255 282500733 Fax: +255 282541484 Email:mwanza@tfda.or.tz

TFDA kanda ya ziwa yasimamia zoezi la uteketezaji wa bidhaa za dawa za Serikali zilizokwisha muda wake.

TFDA Ofisi ya Kanda ya Ziwa ilisimamia zoezi la uteketezaji wa bidhaa za dawa na vifaa tiba katika Manispaa ya Bukoba, na Halmashauri ya Wilaya ya Karagwe.
Zeozi hilo lilifanyika tarehe 30/09/213 hadi tarehe 03/10/2013.Dawa zenye uzito wa Tani 1.6 thamani ya TZS19,698,855/-.mali ya Hospitali ya Mkoa wa Kagera,. uzito wa Tani 3.15.na thamani TZS93,118,589.05/-Mali ya Halmashauri ya Wilaya Bukoba na uzito wa Tani 6.0 na thamani TZS65,629,010/- Mali ya Halmashauri ya wilaya ya Karagwe zilizokwisha muda wa matumizi ambazo zimekusanywa kwa kipindi kirefu sana zaidi ya miaka kumi ziliteketezwa.




Pichani  ni bidhaa za dawa na vifaa tiba zikiwa zinaandaliwa  kuwekwa katika INCENERATOR kwa ajili ya kuteketezwa
 
                                            .




Pichani ni bidhaa za dawa ambazo tayari zimeshaandaliwa kwa ajili ya kufukiwa katika ardhi.Dawa husika huchanganwa na chokaa na cement na kufanyika udongo mgumu tayari kufukiwa.


Pichani ni bidhaa za dawa ambazo zimetengwa na kufunganshwa tayari kwa kuchomwa.









Pichani ni Kikao cha Kamati ya kuteketeza bidhaa iliyoundwa na Mfamasia wa Mkoa,Mganga Mkuu wa Mkoa, Mhakiki Mali wa Mkoa, Afisa Usalama wa Taifa, Afisa wa Polisi, Mhakiki Mali kutoka Wizara ya fedha, Mwakilishi wa Mfamasia Mkuu wa Serikali , Mkaguzi wa Dawa Ofisi ya Kanda, TFDA, Afisa Afya wa Mkoa na wajumbe kutoka kwa Wafadhili (John Snow Inc)


TFDA kanda ya ziwa yateketeza bidhaa zisizokidhi viwango vya ubora

TFDA ofisi ya Kanda ya Ziwa imeteketeza bidhaa za vipodozi,dawa,vifaa tiba na chakula visivyokidhi vigezo vya ubora baada ya kukamatwa katika soko katika ukaguzi wa dawa uliofanyika tarere 11-19 mwezi julai 2013, ukaguzi wa vipodozi uliofanyika tarehe 22-29 mwezi Julai 2013 na ukaguzi wa kawaida kwa mwezi August.
Jumla ya bidhaa zenye uzito wa Tani 3.5 na thamani ya TZS 26,647,550 ziliteketezwa katika dampo la Jiji lililoko Buhongwa katika Manispaa ya Nyamagana.

watumishi wa Ofisi ya Kanda ya Ziwa wakiwa wanajiandaa na maandamano ya siku ya wafanyakazi







Pichani Wafanyakazi wa ofisi ya Kanda ya Ziwa wakiwa mbele ya ofisi ya kanda wanajiandaa kwenda kwenye maandamano ya Siku ya wafanyakazi Mei Mosi mwaka 2013

uteketezaji wa bidhaa kwa hiari


Wadau wanaojihusiha na biasahara ya bidhaa za chakula,dawa ,vifaa tiba na vipodozi wanapaswa kusalimisha kwa hiari bidhaa ambaza  hazifai kwa matumizi ,zilizokwisha muda wake na ambazo zimepungua ubora zikiwa sokoni ili kuweza kuteketezwa.
Pichani ni bidhaa za dawa na vifaa tiba za duka mojawapo la dawa Mwanza mjini zikiwa zinateketezwa chini ya usimamizi wa TFDA, TRA, Polisi n.k

Watumishi wa TFDA ofisi ya Kanda ya Ziwa ,wakiwa katika sherehe za siku ya wafanyakazi(Mei Mosi) Katika uwanja wa CCM Kirumba.


Pichani watumishi wa ofisi ya Kanda ya Ziwa,TFDA.wakiwa katika uwanja wa CCM Kirumba katika Sikukukuu ya wafanyakazi ya Mei Mosi


Shehena ya vipodozi vyenye viambata vya sumu vikiwa vinataka kusafirishwa kwenda Dar es salaam


Vipodozi vyenye viambata vya sumu vikiwa katika lori tayari kusafirishwa kwenda Dar es salaam. Vipodozi hivyo vilikamatwa na wakaguzi kufuatia msako mkali unaoendelea wa kukamata bidhaa zote za chakula,Dawa ,Vipodozi na Vifaa tiba ambazo hazijakidhi matakwa ya Sheria ya Chakula ,Dawa na Vipodozi namba 1 ya Mwaka 2003.

SHEHENA YA VIPODOZI VILIVYOPIGWA MARUFUKU KUTOKA NJE YA NCHI VIMEKAMATWA JIJINI MWANZA



Mkaguzi wa Dawa wa Ofisi ya Kanda ya Ziwa akiwa anaorodhesha bidhaa za vipodozi vilivyopigwa marufuku kufuatia kukamatwa kwa gari ambalo lilikua lina mzigo huo ukiwa umeingia nchini. Shehena hiyo ya vipodozi hivyo ilikua inaandaliwa kusafirishwa kwenda Jijini Dar es salaam.
Vipodozi vyote vilikamatwa na wakaguzi na zoezi la uteketezaji linaandaliwa kufanyika katika Dampo ya Buhongwa tarehe 24 Aprili 2013
Powered by Blogger.